ERASTO BLOG

MICHEZO NA BURUDANI

Recent Posts

LightBlog

Breaking

Wednesday, August 8, 2018

Majuto afaliki dunia

Breaking News: Mzee King Majuto Afariki Dunia

globalpublishers.co.tz

Aug 8, 2018 9:25 PM

Breaking News: Mzee King Majuto Afariki Dunia

MSANII nguli wa vichekesho Tanzania, Amri Athuman ‘Mzee King Majuto’ amefariki dunia majira ya saa 2:00 usiku huu wa Agosti 8, 2018 katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.

Mtoto wa marehemu aitwaye Abuu amethibitisha kifo cha baba yake.

Pia, mchekeshaji Joti ndio wa kwanza kutoa taarifa hizo kupitia mtandao wa instagram.

“R.I.P King Majuto Umetuachia Maumivu Makubwa sana katika Tasnia ya Comedy Tanzania, sisi wanao, tutakukumbuka kwa kazi zako, upendo wako, tabasamu lako Daima milele, tulikupenda sana ila Mungu amekupenda zaidi, pumzika kwa Amani Mzee wetu,” amendika Joti.

Mzee Majuto alizaliwa mwaka 1948 mkoani Tanga na kusoma Shule Msambwini, mkoani humo, alianza kuigiza 1958 akiwa na umri wa miaka 10.

Hivi karibuni Mzee Majuto alisafirishwa na kupelekwa nchini India ambako alipatiwa matibabu na kurejea nchini ambapo alipelekwa Muhimbili kuendelea na tiba yake.

Mzee Majuto ndiye alikuwa muigizaji wa kwanza kuandaa kazi zake katika mikanda na kuuza akiwa na Tanzania Film Company ( TFC), alikuwa mwigizaji mwenye mashabiki wengi kutokana maonyesho mbalimbali, vichekesho vyake aliyoshiriki nchi mbalimbali.

Tazama yote

Fungua Opera News ili kusoma zaidi

Follow fav football team, live score & comentary

Ripoti tatizo

23Chukia

COPY SUCCESS

No comments:

Post a Comment