ERASTO BLOG

MICHEZO NA BURUDANI

Recent Posts

LightBlog

Breaking

Friday, August 3, 2018

Hii ndio sababu zawadi ya Miss Lake Zone kugomewa

Hii ndio sababu zawadi ya Miss Lake Zone kugomewa

dar24.com

Aug 3, 2018 1:04 PM

Comments Off on Hii ndio sababu zawadi ya Miss Lake Zone kugomewa

Gari aina ya Passo lenye thamani ya Shilingi Milioni 8 za kitanzania lililoandaliwa kama zawadi kwa mrembo atakayeshinda shindano la Miss Lake Zone limekataliwa na waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, The Look Company kwa kile walichosema kuwa haliendani na hadhi ya mashindano hayo.

Hata hivyo tayari waandaaji wa shindano la Miss Lake Zone wameandikiwa barua inayowataka kutafuta zawadi nyingine bora zaidi na barua hiyo tayari imetumwa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA).

”Zawadi hiyo haiendani na hadhi ya mashindano najua wanajitahidi kutoa zawadi kubwa lakini kusema ukweli hatujaafiki” amesema Basilla Mwanukuzi ambaye ni Mkurugenzi wa The Look Company.

Aidha amesema waandaaji wa chini wa shindano hilo hawana ulazima wa kutoa zawadi kubwa bali kuwatafuta wasichana wenye vigezo na kuendesha shindano hilo kwa uweledi.

”Zawadi kubwa za magari inabidi watuachie sisi huku juu siyo kulazimisha, ninajua wana nia njema lakini hili hatukubaliani nalo” ameongezea Basilla.

Hata hivyo Fred Kikoti ambaye ni mwandaaji wa shindano la Miss Lake Zone amesema hana taarifa yeyote ya kukataliwa kwa zawadi hiyo.

Shindano la kumsaka Miss Lake Zone linatarajiwa kufanyika siku ya Kesho Agosti 4, 2018  jijini Mwanza ambapo warembo 15 watachuana vikali kutafuta zawadi ambayo hadi sasa haijafahamika rasmi mara baada ya The Look kuitolea nje zawadi iliyoandaliwa hapo awali.

Tazama yote

Fungua Opera News ili kusoma zaidi

Offline reading without Internet. Download 1000+ news in just 10 seconds.

Ripoti tatizo

194Chukia

COPY SUCCESS

No comments:

Post a Comment