ERASTO BLOG

MICHEZO NA BURUDANI

Recent Posts

LightBlog

Breaking

Saturday, July 7, 2018

Ronaldo alivyoipandisha thamani Juventus ndani ya siku tatu

Staa wa soka wa kimataifa wa Ureno anayeichezea club ya Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo jina lake bado linazidi kuchukua headlines kila kukicha kutokana na ishu yake ya kuhusishwa kwake kwenda kujiunga na club ya Juventus ya Italia.

Ronaldo ambaye alikuwa Urusi akiiwakilisha Ureno katika fainali za Kombe la Dunia, kwa sasa anahusishwa kwa karibu kukaribia kujiunga na club ya Juventus ya Italia, hivyo report kutoka mtandao wa Bleacher Report unaeleza kuwa kufuatia tetesi hizo Ronaldo ameiongezea thamani Juventus.

Juventus hadi kufikia July 2 ilikuwa na thamani ya euro milioni 665 lakini baada ya kuanza kuhusishwa na kumsajili Ronaldo July 5 thamani ya club hiyo imefikia euro milioni 825, kuna tetesi nyingi kuwa Ronaldo atajiunga na Juventus kwa dau la euro milioni 88 kama Real Madrid wataikubali ofa ya Juventus.

No comments:

Post a Comment