Comments Off on Nauli za ndege mpya Boeing 787-8 Dreamliner hizi hapa, sawa na bure
Kufuatia ujio wa ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner ambayo inatarajiwa kuanza safari zake wiki tatu zijazo tayari nauli za kupanda ndege hiyo zimeweka bayana ambapo gharama zimetajwa kuanzia Shilingi 93,000 tu kwa safari moja.
Hata hivyo ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 262 inatarajia kuanza safari zake Julai 29, 2018 kuanzia Dar es salaam kuelekea Kilimanjaro na kisha kuelekea Mwanza na kutoka Mwanza ndege hiyo itakuwa inaruka kuelekea Kilimanjaro na kurudi jijini Dar es salaam kila siku kwa mwezi mzima.
Hizi ndio gharama za nauli ya ndege mpya Boeing 787-8 Dreamliner.
Dar – Mwanza shilingi 113,000 pamoja na kodi kwa sufari moja, lakini kwenda na kurudi ni shilingi 206,000.
Kilimanjaro – Mwanza shilingi 93,000 kwa safari moja, kwenda na kurudi ni shilingi 1666,000
Dar es salaam – Kilimanjaro shilingi 98,000 kwa safari moja, kwenda na kurudi ni shilingi 176,000
Aidha ndege hiyo inatarajiwa kurushwa na marubani 8, ilitua jijini Dar es salaam Jumapili iliyopita na kupokelewa na watanzania wakiongzwa na Rais John Pombe Magufuli.
Tazama yote
Fungua Opera News ili kusoma zaidi
Follow fav football team, live score & comentary
10
Chukia
0762995785
COPY SUCCESS
No comments:
Post a Comment