by erasto
Diamond Platnumz akiwa na watoto wake Tiffah na Nillan
Kama wewe ni shabiki wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz au pengine unawakubali wasanii wengine wa kutoka WCB basi habari hii ikufikie.
Habari njema ni kwamba mwezi ujao mwezi Agosti 06, 2018 ndio mwezi ambao mtoto wa kwanza wa Diamond Platnumz, Tiffah anasherehekea siku yake ya kuzaliwa na Diamond ameahidi kusherehekea kitofauti kidogo ambapo amesema kuwa atawaalika mashabiki wake 30 kwenye Party hiyo itakayofanyika Afrika Kusini.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond amesema kuwa mashabiki hao atawalipia gharama zote za nauli kwenda na kurudi na huduma za malazi.
“Watu 30 Wenye Bahati ntawalipia Ndege na Malazi kwenda Kusheherekea na @princess_tiffah Uzaliwa wake South Africa….. wanyumbani kama kawa LIVE on @wasafitv“ameandika Diamond.
Party hiyo pia itarushwa live kupitia kituo chake cha runinga cha Wasafi TV na itaambatana na Birthday Party ya Romy Jons.
Hata hivyo, haijaelezwa ni njia zipi atatumia kuwapata mashabiki hao 30 lakini mashabiki wake endeleeni kumfuatilia kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kwani huko ndiko atakakotangaza vigezo na masharti.
The post Diamond Platnumz atangaza habari njema kwa mashabiki wa WCBappeared first on Bongo5.com.
Tazama yote
Fungua Opera News ili kusoma zaidi
Offline reading without Internet. Download 1000+ news in just 10 seconds.
119
Chukia
COPY SUCCESS
No comments:
Post a Comment