Taarifa ya Habari za Ulimwengu kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW
HABARI
27.06.2018 | 15:00
Machar na Kiir wasaini makubaliano ya amani
Viongozi mahasimu wa kisiasa nchini Sudan Kusini rais Salva Kiir na kiongozi wa waasi, Rieck Machar wametiliana saini makubaliano ya amani mjini Khartoum ambapo chini ya makubaliano hayo wameridhia kutekeleza katika kipindi cha saa 72 hatua ya kudumu ya kusitisha mapigano. Hatua hiyo imeibua matumaini kwamba mkataba huo utahitimisha vita vya muda mrefu vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo. Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Al-Dierdiry Ahmed ametangaza mwafaka huo baada ya kufanyika mazungumzo katika mji mkuu wa Sudan Khartoum. Amesema pande zote zimekubaliana usitishwaji wa kudumu wa mapigano utakaoanza ndani ya masaa 72. Kiir na Machar wamesaini waraka mbele ya rais wa Sudan Omar Al Bashir. Baada ya kutiliana saini Kiir alisema hii ni siku ambayo raia wengi wa Sudan Kusini waliitarajia. Machar alisema usitishwaji huu wa mapigano ni lazima uwe mwelekeo wa kumaliza mapigano. Juhudi mpya za amani za Sudan Kusini zilianzishwa na viongozi wa Afrika Mashariki.
Seehofer atoa masharti ya kupokea wahamiaji
Jinping azungumza na Mattis
Poland yageuza sheria yake kuhusu mauaji ya Holocoust
Putin Bolton wajadili mahusiano ya Urusi na Marekani
Congo, Mali na Yemen yaingizwa orodha mbaya
Mahakama yasimamisha utenganisho wa familia Marekani
Sikiliza matangazo ya moja kwa moja
Sikiliza matangazo ya moja kwa moja
Taarifa ya Habari, saa 12:00 (Afrika Mashariki)
Matangazo ya Asubuhi, saa 12:08 (Afrika Mashariki)
Matangazo ya Mchana, saa 7:00 (Afrika Mashariki)
dakika (0)
No comments:
Post a Comment